Sunday, February 26, 2017

Jinsi Ya Kutumia Mbinu Ya Utabiri Kumvunja Nguvu Mwanamke Ili Abaki Na Wewe Milele

Jinsi Ya Kutumia Mbinu Ya Utabiri Kumvunja Nguvu Mwanamke Ili Abaki Na Wewe Milele

Ok, hebu tuanze kwa kuuliza maswali. Je ushawahi kuwa na girl friend? Kama huna girlfriend mpaka siku ya leo unangojea nini?
Na kama umekuwa na girlfriend muda huu wote, je wewe na huyu girlfriend wako mnaishi vipi? Je mnazozana, mnakosana, ama hamuelewani?

Katika mahusiano haswa inapotokea kuwa nyote wawili mnapendana lakini kuna mmoja wenu hajaridhika na mwenzake basi mara nyingi ukifanya uchunguzi utakuja kugundua kuwa mmoja kati ya nyinyi wawili huwa ana mchepuko/ mpango wa kando.

Na mara nyingi inauma sana iwapo huyo ambaye anakuwa na mpango wa kando ni mpenzi wako, na mbaya zaidi ni pale ambapo bado unampenda huyu mpenzi wako.

Kwa kueleza kifupi ni kuwa umegundua kuwa mpenzi wako ana mpenzi wa kando na wewe hujaridhika na hio hatua ya yeye kutaka kukuacha na kumfuata huyo mwingine.

Ikifikia hapa utachukua hatua gani ili asikuache? Hapa ndipo hii mbinu ya ‘utabiri’ inaingia kati.

Hebu tuuchukulie huu mfano. Wakati mteja ameingia katika duka flani anataka kununua bidhaa lakini hajaridhishwa na bidhaa anazoziona na anataka kuenda katika duka la pili huwa mhudumu kwa kawaida hamkatizi tamaa yake ya kuenda katika duka la pili bali humpa mawazo na hutabiri kile ambacho atapatana nacho katika duka la pili. Kwa kawaida atamwambia, “Jiskie huru kuenda katika duka flani na flani , lakini kumbuka kuwa maduka hayo huwa bei zao ziko juu kupita kiasi, ama hutapata bidhaa mahususi unayotafuta, ama utadhulumiwa nk.

So, huyu mhudumu amefanya nini hapa? Rahisi! Kama huyu mteja ameshawishika na kuamua kubaki hapo, atakuwa ameshinda. Kama huyu mteja ameamua kuenda katika duka la pili, na kugundua kuwa kile alichoambiwa ni kweli na kurudi tena, atakuwa pia ameshinda. Na kama ataenda na hatarudi, basi hakutakuwa na utofauti wowote kama vile awali.

Sasa hebu fikiria kidogo jinsi ya kuitumia mbinu hii kwa girlfriend wako ama kwa mpenzi wako. Unaweza kutumia hii mbinu kumvunja nguvu iwapo kuna mwanaume flani yeyote pale ambaye anamtatiza kihisia.

Kwa mfano unaweza kumwambia, “Uko huru kuendelea na yeye, ni kawaida, inakubalika. Lakini najua kufikia hadi sasa umeshagundua kuwa huyo unayemfuata ana tabia ambayo si nzuri kwako, tabia ambayo inakutatiza na kukusumbua... na utapata kugundua tabia nyingine mbaya zaidi kadri ambapo utazidi kuendelea kuwa na yeye.”

Hapa moja kwa moja atajaribu kuvuta taswira za tabia zozote mbaya ambazo ashawahi kuzishuhudia kutoka kwa huyu mwanaume.
 Kumbuka utabiri unaoutoa hapa utakuwa hauna uhusiano mmoja kwa moja na huyu mwanaume bali unasema na kubahatisha tu. Lakini kwa mwanamke atadhania kuwa tayari unamjua huyu mwanaume na tabia zake.

So moja kwa moja kama huyu mwanamke kweli ana hisia kwako anaweza kubadili msimamo wake na kukubali kuendelea na wewe.
Upo!?

Thursday, February 16, 2017

HATUA KUMI ZA KUCHAGUA MCHUMBA

HATUA KUMI ZA KUCHAGUA MCHUMBA


Wengi wamejikuta wakiitwa wahuni kutokana na kuwa na uhusiano wa kimapenzi na makundi ya wanaume au wanawake. Hata hivyo wachunguzi wa masuala ya mapenzi wanasema idadi kubwa ya wapenzi si kigezo sahihi cha kupima tabia ya mtu na kumhusisha na uhuni.

Watalaam hao wanataja safari ya kupata chaguo halisi la mwanaume/mwanamke wa maisha ndiyo inayowaponza wengi kiasi cha kujikuta wameingia katika kashfa ya kuwa na uhusiano na dazeni ya wapenzi.

Wanasema msichana/mvulana anayeingia katika uwanja wa mapenzi kwa kuwa na hisia za kufanya ngono, hukosa umakini wa nani anafaa kuwa mpenzi wake kutokana na kukosa elimu ya uhusiano kutoka kwa wazazi wake.

Kwa mantiki hiyo, bila upembuzi wa kina, mtu asiye na elimu ya jinsi ya kumpata mpenzi wa kweli hujikuta ameangukia kwa mwanaume/mwanamke asiyemfaa, ambapo baadaye huamua kuachana na huyo na kwenda kwa mwingine kujaribu bahati tena ya kupata penzi la kweli.

Zinatajwa zawadi, hitaji la kusaidiwa kimaisha, mvuto wa kimahaba na mazoea kuwa ni vichocheo vinavyowaangusha wengi kwenye mapenzi na wasiowafaa.

Ukweli ni kwamba mtu aliyenaswa kwa ‘ujinga’, huwa hakatwi kiu ya penzi na mwanaume/mwanamke asiye chaguo sahihi la maisha yake. Hivyo hufikia maamuzi ya kujiingiza katika uhusiano mpya mara 2,3,4,5 na kujikuta wakiambulia wanaume/wanawake wale wale wasio sahihi kwake.

Mwanamnke mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Suzzy aliwahi kuniomba ushauri, akasema amechoka kuchezewa, maana kila mwanaume anayempata anakuwa si chaguo lake. Lakini kibaya zaidi kuachia ngazi au kutemwa huku akiwa tayari ameshafanya mapenzi na wanaume hao.

Nia ya swali lake ilikuwa ni kuniomba njia za kumtambua mwanaume mkweli bila kufanya naye mapenzi? Aliuliza hivyo huku akiwa na hoja kuwa wanaume wengi hawako tayari kuwa na uhusiano na msichana bila kufanya naye mapenzi na wakati huo huo huficha tabia zao chafu wakilenga kumnasa wamtakaye.


Binafsi nafahamu kuwa kuna wanawake/wanawake wengi ambao hujiingiza katika mapenzi kwa kutekwa na hadaa za mwili na kujikuta wanacheza mchezo wa kitoto wa pata potea.

Ni madhumuni ya somo hili kufundisha vigezo vya kumpata mwanaume/mwanamke halisi wa maisha, bila kufanya naye mapenzi. Njia hii ina faida kwa pande zote mbili yaani kwa mwanamke na mwanaume kwani kuacha au kuachwa bila kufanya mapenzi ni bora kuliko kuwa muonjaji, tabia ambayo huathiri kisaikolojia na ni hatari kwa afya.

Ifuatavyo ni njia ya kisaikolojia ambayo mwanamke anaweza kutumia kumpata mwanaume mwenye kumfaa bila kufanya naye mapenzi tena ni jibu sahihi la kuondokana na mchezo wa kubahatisha kwa wanaume wanaosaka wapenzi wa kweli na si taksi bubu ambazo mchana huweka namba za njano usiku nyeusi.

KWANZA- Ni ya mwanamke/mwanaume mwenyewe kujifahamu na kufahamu vigezo vya mpenzi anayemhitaji katika maisha yake. Ifahamike kuwa kila mwanaume ana wake na kila mwanamke anaye wake wa maisha pia. Hivyo asiyekufaa wewe anawafaa wengine, kinachotakiwa ni wewe kujitambua kwanza ili umtambue umtakaye.

Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakachezewe na kuumizwa moyo bure.

PILI- Ni kuketi chini na kuorodhesha vigezo stahili vya mwanaume/mwanamke unayemtaka. Baada ya hapo orodhesha tena kasoro za mwanaume/mwanamke unazoweza kuzivumilia na zile ambazo huwezi kuzivumilia kabisa. Hii inatokana na ukweli kwamba mwanadamu hajakamilika, ana upungufu wake.

TATU- Anza kumsaka kwa kutumia milango ya fahamu. Cha kufanya hapa ni kuruhusu macho yawaone wanaume/wanawake na kuwatathmini kwa maumbile yao ya nje na kisha kupata majibu kutoka moyoni juu ya kuvutia kwao ambako hutambulika kwa moyo kurithika na mwili kusisimka.

NNE - Kuanzisha safari ya kuchunguza tabia za nje na za ndani kivitendo. Hapa suala la ukaribu baina ya mwanaume na mwanamke linahitajika. Msingi unaotajwa hapa ni kujenga mazoea ya kawaida yasiyokuwa na masuala ya kimapenzi na ngono. Kutambuana, , viwango vya elimu, kabila na makundi ya marafiki ni mambo ya kuzingatia.

Katika uchunguzi huu mwanamke/mwanaume anayetafuta mpenzi hana budi kupitia na kumlinganisha huyo aliyempata na vigezo alivyojiwekea. Zoezi hili liendane na kuweka alama ya pata kila anapobaini kuwa mwanaume/mwanamke anayemchunguza amepata moja ya vigezo vyake. Lakini pia aweke alama ya kosa kwa kila kasoro anayoivumilia na ile asiyoivumilia.

TANO - Ajipe muda wa kutosha kati ya miezi sita na mwaka kumchunguza huyo mwanaume, kisha aketi chini na aanze kujumlisha alama za vigezo alivyovijiwekea na jinsi mwanaume huyo alivyopata au kukosa.

Ikibainika mwanaume aliyechaguliwa amepata zaidi ya nusu ya alama ya vigezo vilivyowekwa, basi ujue kuwa anafaa. Kuhusu alama chache alizikosa anaweza kusaidia kuzikamilisha polepole wakati wa maisha ya ndoa.

Lakini angalizo kubwa kabisa ni kwamba mwanaume/mwanamke akionekana kuanguka katika kasoro zisizoweza kuvumilia kwa zaidi ya alama tatu. Yaani kwa mfano ni mlevi, mwizi, muongo, mbishi na katika hizo kashindwa 3, huyu hafai, ni vema akawekwa kando kwani huwezi kubeba kero 3 kwa pamoja katika maisha.

SITA - Kusajili mapenzi yenye malengo yanayotekelezeka. Lazima baada ya kuchunguzana kwa kina wapenzi watengeneze muongozo wa mapenzi yao. Wasiwe kama wanyama, lazima mipango ya wapi wametoka walipo na wanapokwenda.

Hata hivyo watalaam wanasema lazima wapenzi wapime umakini wao kwa vitendo. Kama wamekubaliana kuoana, suala la mume kwenda kujitambulisha kwa wakwe na hatua ya kuiendea ndoa ionekane. Usiri usiwepo tena. Kila mmoja amuone mwenzake kama sehemu ya maisha yake na mara zote wasaidiane kwa ukaribu.

SABA - Ni vema ndugu wakashirikishwa ili kuwapa nafasi na wao ya kuamua kama mapenzi hayo ni budi yakaendelea au yakasitishwa. Ni ukweli ulio wazi kwamba licha ya wengi kupuuza maamuzi ya ndugu kwa madai ya kuwa hawana nafasi kwa wapenda nao, lakini uchunguzi unaonesha kuwa wapenzi wengi huacha kutokana na sumu za ndugu hasa pale wanapokuwa wameonesha kutounga mkono uhusiano wa wanaotaka kuoana

NANE - Hatua hii ni ya kuweza kuzungumzia ufanyaji mapenzi, hapa nina maana kama wapenzi wamejizuia kwa muda mrefu na wanahisi kuchoka wanaweza kujadiliana kuhusu hilo na kuamua ufanyaji huo wa mapenzi una lengo gani, kama ni kuburudisha miili basi suala la afya na uzazi salama litazamwe.

TISA - Kutimizwa kwa ahadi ya kuoana ni hatua ya tisa ambayo nayo si busara ikachukua muda mwingi kutekelezeka, kwani ucheleweshaji mwingi wa ndoa nao huvunja moyo na mara nyingine umewafanya wengi kutoaminiana.

KUMI - Kuamua kuwa mwili mmoja kwa kuvumilia na kuwa tayari kukabiliana na changamoto zote za maisha ukiwemo mkwamo na dhiki ambazo huchangia sana ndoa nyingi kuvunjika. Hapa pia ni wajibu wa wanandoa kuchukuliana udhaifu na kusaidia, kuwa tayari kujifunza na kujali zaidi upendo kuliko hisia za mwili ambazo wakati mwingine hudanganya na hivyo kumfanya mwanandoa asivutiwe na mwenzake.

Mwisho ni kwamba kanuni hizi huwafaa watu wazima mapenzi ya kitoto hayawezi kujenga misingi hii imara mara nyingi ni kudanganyana, kuharibiana maisha, kupeana mimba na maradhi.


Thursday, February 9, 2017

Jinsi ya kuifanya ngozi yako kuwa na afya na mng'ao kwa kutumia vitu vya asili

Urembo: Jinsi ya kuifanya ngozi yako kuwa na afya na mng'ao kwa kutumia vitu vya asili



Uzuri wa ngozi sio rangi tu bali ni
muonekano wa ngozi yenyewe kwamba ina afya na mng'ao unaoashiria afya njema.
Leo tushirikishane jinsi ya kufanya facial treatment kwa kutumia vitu vya jikoni kama kiini cha yai,machicha ya nazi,tango na limao.Treatment hii inaweza kufanyika Mara moja kwa wiki au kila baada ya wiki mbili, unaweza kufanya hata mara moja kwa mwezi ukipata nafasi kama unakuwa busy sana lkn matokeo mazuri utayashuhudia.

Andaa maji masafi yenye joto kiasi unachomudu ktk ngozi yako, osha uso wako kwa hayo maji safi .
Kama una ngozi kavu au ya kati chukua kipande cha tango kidogo na upake yale maji yake usoni,



 kwa wenye ngozi ya mafuta unaweza kutumia kipande cha limao kwa kupaka maji yake.


Chukua pamba au kitambaa laini na futa maji ya matunda usoni kwa mtindo wa kusafisha taratibu usoni.
Chukua machicha ya nazi na Anza kuusugua uso  na shingoni taratibu Mpaka uridhike uso wote umepitiwa na machicha yako hasa unapoona unang'aa kwa mafuta kidogo yaliyotoka kwenye nazi. Kisha pukuta yale machicha ubaki na uso unaong'aa bila vitu vyeupe yaani machicha.


Chukua kiini cha yai inapendeza ukitumia la kienyeji, au la kisasa lenye kiini cha njano iliyokolea angalau. Ili kiini kisijichanganye na ute wakati wa kupasua ,ligonge yai upande mmoja sio katikati na limimine ktk chombo mithili ya sahani ambayo unaona kiini katikati kisha unakichota na kuweka kando. Paka ule uji mzito wa njano wa kiini uso mzima bila kusahau shingoni na nyuma ya masikio na ngozi ya masikio.


Baada ya kupaka kiini cha yai unaweza kuendelea na shughuli zako huku likiendelea kukauka,linapokauka ngozi yako inakuwa kama inajivuta vuta.Baada ya kule kuvuta kuisha inamaanisha yai limekauka kabisa. Osha uso wako kwa maji safi maji yawe ya baridi sasa.Jinsi inavyofanya kaziTango au limao hutumika kama cleanser, unapokuja kujifuta taratibu unaondoa uchafu katika ngozi yako.Machicha ya nazi yanatumika kama scrub, yanaondoa seli zilizokufa, kuifanya ngozi kuwa laini na kuipa mngao.Kiini cha yai hapa kinatumika kama maski, matundu ya ngozi yanajifunga vizuri na kinaipa ngozi yako lishe kutokana na vitamins zilizomo kwenye kiini cha yai kama vitamin E.Mwishoni unanawa na maji baridi ili kuruhusu matundu ya ngozi kujifunga na kuifanya ngozi ijiweke sawasawa.Faida za hii treatmentHusaidia kutibu na kuikinga ngozi na chunusi,Kuipa ngozi mng'ao bila kutumia kemikali za sumu,Husaidia kupunguza mikunjo ktk ngozi yako(wrinkles zinapungua)Gharama ndogo kuifanya

Wednesday, February 8, 2017

majina 65 yaliyotajwa leo sakata ya madawa ya kulevya

Mbowe,Manji ,Idd Azan,Mch.Gwajima ni  kati ya majina  65 yaliyotajwa leo sakata ya madawa ya kulevya #RC Makondo
MMILIKI WA SLIPWAY...

YATCH CLUB..
MMI SALEH..

MWINYI MACHAPTA

BALOZI
KIBOKO WA MBEZI YA CHIN
ALLY FIDHI MBEZI CHIN

IDDI AZAN

MBOWE

BOSS CHIZENGA

MASANGA,Bunju

Deo mchanga

Mahalifu

Abel mfundo

Kizza

Kitwana

Hashiri

Halidi mwarabu

Nassoro selem

Hussein mwarabu

Hussein pamba kali

Gwajima

Yusuph manji

Mmiliki wa cassino la Sea Cliff..

Petroleum limited

GPB


Monday, February 6, 2017

SIFA KUMI ZA MWANAMKE ANAYEJITAMBUA.....

SIFA KUMI ZA MWANAMKE ANAYEJITAMBUA.....

1. Wanaume huchagua wanawake kama vile mtu anachagua yeboyebo zilizotandazwa chini sokoni na kwa mwanaume yeyote ataokota tu zile ambazo ziko karibu yake wakati mwingine hata kama hazimtoshi. Lakini kwa mwanamke anayejitambua na anayejua thamani yake atakuwa sawa na kiatu kizuri ambacho kimetundikwa dukani juu kabisa tena kwenye duka la kioo ambacho hakipatwi hata na vumbi. Anajua thamani yake hivyo atamfanya mwanaume amhangaikie kumfuata dukani na kumchagua kwa heshima, hata jirahisisha na kuruhusu kutandazwa tandazwa chini.
2. Mwanamke anayejitambua anapaswa kujua kuwa mahusiano yanachangamoto lakini angalau asilimia 8o ya muda wenu muutumie mkifanya mambo yakuwapa furaha, kama mnatumia zaidi ya asilimia ishirini ya muda wenu kugombana basi jua uhusiano wenu hauendi popote, jitathimini kama unamhitaji huyo mtu au la?
3. Mwanamke anayejitambua hujipenda yeye mwenyewe kwanza kabla ya kumpenda mwanaume, hii ni kutokana na ukweli kuwa, kama hujipendi hata kama ukipendwa vipi huwezi furahia upendo huo.
4. Mwanamke anayejitambua anajua pia ni kitu gani anakitaka kwa mwanaume na anahakikisha anakipata. Kama hujui unachokitaka kwake hata ukikipata bado utajihisi hujakamilika, hembu jiulize sasa unataka nini kwenye mahusiano uliyonayo sasa.
5. Mwanamke anayejitambua halinganishi mahusiano yake ya sasa na yazamani, au mahusiano yake na mahusiano ya rafiki yake. Huamua kuwa na furaha sasa bila kujali huko nyuma maisha yalikuwaje, husahau yaliyopita na hahangaishwi na mambo yanayofanywa na wengine.
6. Mwanamke anayejitambua huchagua aina ya mwaname anayemtaka na si kuchukua tu kila mwanaume kwakuwa tu ni mpweke au anahisi umri umeenda.
7. Mwanamke anayejitambua hujitoa kimwili kwa mwanaume pale anapohisi kuwa yuko tayari kufanya hivyo na si kwakuwa anaogopa kumpoteza mwanaume, kwani anajua thamani yake na anajua kama mwanaume anamthamini basi hatajali sana kuhusu ngono bali ataangalia upendo wa kweli.
8. Mwanamke anayejitambua anafahamu kuwa mwanaume si Baba yake, Kaka yake au Bosi wake bali ni rafiki yake, hivyo atamheshimu lakini hatamuogopa na yuko tayari kuongea kuhusu hisia zake. Kwakuwa anajua anachokitaka atamuambia mwenza wake na kwakuwa ni marafiki basi kila mmoja atakuwa huru na mwenzake.
9. Mwanamke anayejitambua anajua kuwa mapenzi si maisha yake bali ni sehemu tu ya maisha yake, hawezi kusumbuliwa na mwanaume kwakua tu anapenda kwani anajua yuko imara vyakutosha kuvumilia upuuzi wa mwanaume yeyote. Ameiweka mbele furaha yaake kuliko ya watu wengine na anapoona hapati anachokitaka basi hujitoa mara moja kwenye aina hiyo ya mahusiano.
10. Mwanamke anayejitambua hawezi kupigania mwanaume kwani anafahamu kuwa mwanaume hachungwi na kama mwanaume anampenda basi hawezi kuhangaika hangaika na wengine. Anafahamu kuwa mwanaume anachepuka kwakuwa anataka na si sababu ya mwanamke mwingine hivyo basi humaliza mambo yake na mwanaume wake na hapotezi muda wake kugombana na mwanamke mwingine kwaajili ya mwanaume

Sunday, February 5, 2017

Madhara ya Kutumia Tishu kwa Wanawake-2

Madhara ya Kutumia Tishu kwa Wanawake-2      




Wiki iliyopita tulianza kujadili mada hii ya madhara ya kiafya ya kutumia tishu kwa mwanamke. Leo tunaendelea kuanzia tulipoishia:

Pia zipo tishu za kisasa ambazo huwa zinakuwa kwenye pakti maalum, zikiwa na kemikali kwa ajili ya kukata harufu na majimaji yenye pafyumu. Hizi huwa na madhara zaidi kwa sababu kemikali zilizopo kwenye tishu hizo, huwa na athari kubwa kwa afya ya viungo vya uzazi.

Matumizi ya tishu, huchangia kwa kiasi kikubwa ugonjwa wa Vaginosis, ambao husababisha mwanamke atokwe na uchafu kwenye sehemu zake za siri. Hii hutokea kwa sababu, katika njia ya haja kubwa, kuna bakteria ambao huwa hawana madhara kwa ajili ya kuulinda mfumo wa utoaji taka mwilini lakini bakteria hao wanapoingia kwenye viungo vya uzazi husababisha madhara.

Kwa kawaida, watumiaji wengi wa tishu, hujifuta kwa kutokea nyuma kuja mbele, jambo ambalo husababisha iwe rahisi kwa bakteria hao kuhamishwa kutoka njia ya haja kubwa mpaka kwenye mfumo wa uzazi na baadaye maambukizi hutokea.

Wataalamu wa afya, wanashauri kwamba, matumizi sahihi ya tishu, yanapaswa kuwa kama ifuatavyo:

-Hakikisha unanunua tishu zenye ubora uliothibitishwa, siku hizi umeibuka mchezo wa kutengeneza bidhaa feki ambazo hazina ubora unaotakiwa, zikiwemo tishu. Unaponunua tishu za kutumia, hakikisha unazingatia ubora na siyo bei.

-Badala ya kutumia tishu kujifuta (rub), unashauriwa kuzitumia kwa namna ya kama unachovya, kwa maana kwamba hujifuti kwa kusugua ngozi yako ili kuondoa hatari ya kupata michubuko.

– Epuka matumizi ya tishu zenye kemikali (wet diapers) au zenye manukato.

-Unapolazimika kutumia tishu kujisafisha (kama hakuna kabisa maji), lazima ujifute kwa mtindo wa kuanzia mbele kwenda nyuma, yaani, badala ya kuanzia kusafisha sehemu ya haja kubwa ndiyo uje kwenye viungo vya uzazi, anzia mbele kwenda nyuma. Hii itakusaidia kujikinga na kusambaza vijidudu vya magonjwa kutoka kwenye mfumo wa haja kubwa kwenda kwenye viungo vya uzazi.

Pendelea kutumia zaidi maji unapomaliza kujisaidia, iwe haja ndogo au kubwa na tishu zitumike kukausha unyevunyevu tu na siyo kuzitegemea kujisafishia kwa sababu hazina uwezo wa kuondoa uchafu wote bila kukusababishia madhara.

Friday, February 3, 2017

UNA MATATIZO YA KUSAHAU? SOMA HAPA

UNA MATATIZO YA KUSAHAU? SOMA HAPA

Kila seli katika mwili wa binadamu inahitaji kupata hewa ya oksijeni na virutubisho vya kutosha ili viungo vya mwili viweze kufanyakazi yake ipasavyo, zikiwemo seli za ubongo (Brain Cells).

Kwa kuwa hewa ya oksijeni na virutubisho hupita kwenye mfumo wa damu, kitu chochote kinachozuia upitaji huo wa damu husababisha seli kuathirika. Ni ukweli ulio wazi kwamba moyo unapokuwa na afya njema ndivyo ubongo nao unavyoweza kufanya kazi yake vizuri.

Ili ubongo wa mtu ufanye kazi vizuri, ni lazima hali ya moyo iwe nzuri pia. Hatua ya kwanza ya kuchukua ili kuwa na moyo wenye afya ni kujipima shinikizo lako la damu, kama haliko sawa, unatakiwa ulishughulikie tatizo hilo kwanza.
Zifuatazo ni hatua unazoweza kuchukua ili kujenga afya bora ya moyo wako na hatimaye ubongo kuwa na kumbukumbu nzuri:

PIMA SHINIKIZO
Pima hali ya shinikizo lako la damu pamoja na kiwango chako cha kolestro mwilini. Ubongo wenye afya unatokana na moyo wenye afya nzuri na vitu hivyo vinategemeana.

PATA MUDA WA KULALA
Pata muda wa kutosha kulala. Utafiti unaonesha kuwa kukosa muda wa kulala huathiri mfumo wa kumbukumbu ya ubongo.

FANYA MAZOEZI
Fanya mazoezi mara kwa mara. Mazoezi ya mara kwa mara yameonesha kupunguza uwezekano wa mtu kupatwa na magonjwa mbalimbali. Fanya mazoezi angalau kila siku kwa dakika 30 tu.

CHANGAMSHA UBONGO
Usiulaze ubongo wako, upe changamoto kwa kufikiri na kutatua mambo kadhaa ya kimaisha, kwa kufanya hivyo utauchangamsha.

USIVUTE SIGARA
Usivute sigara, kwa sababu uvutaji wa sigara huongeza hatari ya mtu kupatwa na ugonjwa wa moyo na husababisha madhara makubwa iwapo damu itashindwa kwenda kwa wingi kwenye ubongo kama inavyotakiwa.

JIPUMZISHE
Pata muda wa kupumzisha akili kwa kutafuta njia za kuondoa msongo wa mawazo katika kichwa chako.

VYAKULA VINAVYOSAIDIA KUONGEZA KUMBUKUMBU
Utafiti ulio angalia uhusiano kati ya kumbukumbu na vyakula, umeonesha kuwa kadri mtu anavyokula aina nyingi ya vyakula asili ndiyo uwezo wa kumbukumbu yake unavyoimarika.

Utafiti wa muda wa miaka 25 uliofanywa katika Chuo Kikuu cha Tiba cha Havard nchini Marekani, uliowahusu zaidi ya watu 13,000, umeonesha kuwa watu waliokula kiasi kikubwa cha mboga mboga kwa miaka mingi, walikuwa na athari ndogo ya kupungukiwa na kumbukumbu baada ya kuzeeka.

Miongoni mwa mboga zenye kiasi kikubwa cha virutubisho vinavyoongeza kumbukumbu ni pamoja na Brokoli, kabichi na maua ya maboga. Zingine ni mboga za kijani kama vile mchicha, majani ya maboga, nk.

Kwa upande wa matunda, aina zote za ‘beri’, zabibu za rangi ya papo (Purple Grapes), tufaha nyekundu (Red Apples) na matunda yanayojulikana kama vitunguu vyekundu (Red Onions).

Halikadhalika vyakula vyenye kiwango kikubwa cha Folic Acid, husaidia sana katika kuongeza kumbukumbu. Mfano wa vyakula hivyo ni pamoja na nafaka zisizo kobolewa, maharagwe meusi, brokoli, ngano, machungwa, n.k.

SAMAKI
Watafiti wa Rush University Medical Centre, Chicago nchini Marekani, walifuatilia watu 3000, wake kwa waume, kwa muda wa miaka sita kuona ni kwa kiasi gani lishe huathiri kumbukumbu ya mtu.

Utafiti huo ulionesha kuwa watu waliokula samaki angalau mara moja kwa wiki, walionesha kupoteza kumbukumbu taratibu kwa asilimia 10 ukilinganisha na wasiokula samaki. Kiasi hicho kiliwapa uwezo wa kufikiri na kuwa na kumbukumbu sawa na kijana waliyemzidi umri wa miaka mitatu.

Thursday, February 2, 2017

KWA NINI MTOTO MCHANGA HATAKIWI KUPEWA MAJI

KWA NINI MTOTO MCHANGA HATAKIWI KUPEWA MAJI


Wakina mama wengi wanakuwa wanajiuliza bila kupata majibu kama ni sahihi kumpa mtoto mchanga maji .Taasisi za afya dunia kama (World health organization) hazishauri mtoto chini ya miezi 6 kunywa maji,sababu tafiti nyingi zimeonyesha kwamba maziwa ya mama au baby formula yanakiasi cha maji ya kutosha kumtosheleza mtoto.


Sababu zinazomfanya mtoto asipewe maji

Maji kuharibu uwezo wa mwili wa mtoto kunyonya virutubisho vya maziwa ya mama ipasavyo.Maji yatamjaza tumbo mtoto kumfanya ashibe na atashindwa kunyonya kwa kiasi kinachotakiwa.Water intoxication-hii ni hali ya mwili kuwa na kiwango kikubwa cha maji na kuadhiri afya ya mtoto anaweza akazimia mara kwa mara na kumpelekea hata kukaa comaMaji sio salama ,mwili wa mtoto bado ni mdogo hauna kinga ya kutosha kupigana bakteria au virus wanao weza patikana kwenye maji.

Mtoto anaweza pewa kiwango kidogo cha maji iwapo

Anaishi eneo lenye joto kali sana ,anaweza pewa vijiko 2-3 vidogo vya chaiMtoto alieanzishiwa kunywa uji mwepesi kabla ya miezi 6 anaweza pewa  vijiko 3-4 vya chai mara 2 kwa siku.



Ushauri
 afyaborakwamtotoWatoto wanaopewa maziwa ya kopo (baby formula) au maziwa ya mama hawana haja ya kupewa maji mpaka watakapo fikisha miezi 6,mama anaenyonyesha anatakiwa kunywa maji kwa wingi isipungue glasi 7-8 kwa siku.Mama anaweza kuzalisha maziwa machache na ikamfanya mtoto asishibe hivyo anaweza kupika uji mwepesi  iwapo mzazi  hana uwezo wa  kuwanunulia maziwa ya kopo ,mtoto anekunywa uji  apewe maji ya kunywa kwa kuzingatia vipimo sahihi vijiko 3-4 mara 2 kwa siku,ili kusaidia mmeng’enyo wa chakula.

Wednesday, February 1, 2017

SIFA 6 ZA MWANAUME ANAYESTAHILI KUWA MUMEO!

SIFA 6 ZA MWANAUME ANAYESTAHILI KUWA MUMEO!


Wiki hii nitazungumzia sifa 6 za mwanaume ambaye anastahili kuwa mumeo. Nafanya hivi ikiwa ni msaada kwa wale ambao wamefikia hatua ya kuingia kwenye ndoa lakini bado wanashindwa kutambua yupi ni sahihi na yupi si sahihi kuitwa mume.

Tufahamu kwamba si kila mwanaume unayekutana naye na ukampenda anafaa kuwa mumeo. Wengine wana mapungufu makubwa ambayo bila kuyabaini na ukaingia kichwakichwa, utakutana na matatizo makubwa.

Kwa maana hiyo basi, sifa hizi sita ambazo nitazizungumzia leo endapo utaziona kwa huyo ambaye macho yako yameganda kwake, fanya maamuzi sahihi ya kumkubalia.

Anakupenda kwa maana ya kukupenda
Unapoingia kwenye maisha ya ndoa, unatarajia kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwenza wako. Wapo wanaume ambao wanaonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga.

Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na demu flani bomba au kuonja tu penzi kisha kuanza visa ili muachane.Kwa nini ni vizuri kumpata mwanaume mwenye mapenzi ya dhati? Hii inatokana na ukweli kwamba kinyume na hivyo, maisha yatakuwa ya migogoro kila siku. Atakufanyia mambo ya kukuumiza kwa kukusaliti bila kujali maumivu utakayopata. Hii yote ni kwa sababu hana mapenzi ya kweli na wewe.

Ndiyo maana unashauriwa kwamba, kabla hata ya kumuonjesha penzi kisha kufanya maamuzi ya kumruhusu aende kwa wazazi wako ili mfunge pingu za maisha, ni vyema ukawa na uthibitisho kwamba anakupenda kwa moyo mmoja.

Hili la tabia ndo’ kila kitu

Linapokuja suala la ndoa, tabia inakuwa kitu cha awali sana kuangaliwa. Hii ni kwa sababu, wapo wanaume ‘handsome’, wenye kazi nzuri na kipato kizuri lakini wanakosa sifa ya kuitwa mume kutokana na tabia zao chafu.

Hakuna mwanamke anayeweza kudiriki kumpa nafasi mwanaume kuwa mume wake wakati ana tabia chafu. Endapo utaangalia uzuri wa sura kisha ukafanya maamuzi ya kuolewa naye, utakuwa umejichimbia kaburi.

Awe anaota mafanikio
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanawake. Wengi hawapendi kabisa kuolewa na mwanaume ambaye hana kazi.
Mwanaume anatakiwa kuwa dereva katika safari ya kusaka mafanikio, sasa kama atakuwa ni mtu wa kukaa kijiweni, kupiga mizinga, mvivu asiyependa kujishughulisha kwa namna yoyote, huyu hafai kupewa nafasi ya kuitwa mume.

Ile dhana ya kukubali kuolewa na mwanaume yoyote ili mradi upate heshima ya kwamba umeolewa, imepitwa na wakati. Mwanaume sahihi ni yule mwenye malengo maishani, anayefikiria nini cha kufanya kwa ajili ya maendeleo yake, mkewe na watoto wao.

Wa shida na raha
Wapo wanaume ambao siyo wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.

Kwa mfano, unaweza kuingia kwenye maisha ya ndoa lakini kwa bahati mbaya ukawa huna kizazi, mwanaume mwenye mapenzi ya kweli na wewe anatakiwa kukuvumilia na kuwa upande wako.
Yule ambaye atakuwa anaungana na dada zake kukushambulia kwa kutozaa, hafai kuwa na wewe kwani yapo mengi yanayoweza kutokea yanayohitaji kuvumiliana.

Kimsingi uvumilivu kwa mwanaume utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanaume mwenye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.

Anayejua thamani ya mke
Wapo wanaume ambao hawajui thamani ya mke na ukiwachunguza utabaini hawafai kuwa waume za watu. Mume sahihi ni yule anayejua kwamba mke ni kitu cha faraja kwenye maisha yake.
Yule anayeamini kwamba, bila mke maisha yake hayawezi kuwa yamekamilika. Wapo ambao wanaamini hata bila wanawake wanaweza kuwa na maisha mazuri.

Mwanaume mwenye dhana hii, ukimpa nafasi kwenye moyo wako na ukaingia naye kwenye maisha ya ndoa, lazima atakuwa mguu ndani, mguu nje. Hataona hatari kukupa talaka hata kwa jambo dogo tu ambalo mnaweza kuongea na mkalimaliza.

Ndiyo maana nikasema, mwanaume sahihi wa kumpa nafasi ya kuwa mumeo ni yule anayejua thamani ya mke, anayeweza kuvumilia yote akijua mke ndiye anayekamilisha maisha yake.

Asiye na tamaa za kijinga
Unaweza kuwa na mpenzi wa kawaida ukiwa na malengo ya kumfanya awe mumeo katika siku za baadaye. Huyu ukigundua ana tamaa, huna sababu ya ‘kumpetipeti’.
Wanaume wenye tamaa za kijinga ndiyo ambao wakishaingia kwenye maisha ya ndoa wanakuwa wepesi kusaliti. Hao hawastahili kuitwa waume za watu.

Mwisho kabisa naomba niseme kwamba, licha ya sifa hizo 6, yapo mambo mengine ambayo ukiyaona kwa mwanaume ambaye ulikuwa unahisi anafaa kuwa mumeo, ni vyema ukapingana na mawazo.
Mwanaume asiyepitwa na sketi, asiyependa kumsikiliza mwenza wake, anayependa kufanya maamuzi bila kutaka kumshirikisha mwenza wake, anayekuwa upande wa ndugu zake unapokuwa kwenye matatizo, asiyejali familia yake, anayekuona wewe si lolote, asiyethamini na kuwaheshimu ndugu na marafiki zako, huyo kaa naye mbali kabisa.

Ni hayo kwa leo

Monday, January 30, 2017

HEBU FANYA HAYA UFURAHIE NDOA YAKO


HEBU FANYA HAYA UFURAHIE NDOA YAKO


1. MAPOKEZI

Anaporudi kutoka kazini, safarini au kwenye shughuli yake yoyote ile, anza kwa salamu nzuri. Mpokee na kumkumbatia huku uso ukiwa na tabasamu la bashasha.
2. MAVAZI

Jipambe na upake manukato kwa ajili yake mpenzi wako. Vaa vizuri nguo ziwe za kuvutia na za kumtega mnapokua chumbani.

3. USAFI WA MWILI.

Ili kumteka akili mumeo inatakiwa ujue kuoga vizuri na ujue kuzisafisha sehemu nyeti  vizuri na ikiwezekana ipake misk au ifukize udi,japo si shauri Sana matumizi ya miski sehemu nyeti

4. JUA NAMNA YA KUZUNGUMZA NA MUMEO

Unapoanza kuzungumza naye anza na mambo au taarifa nzuri, na kama kuna taarifa mbaya subiri mpaka ale apumzike ndio umuambie.

5. SAUTI

Pendezeshe na uilainishe sauti yako kwa ajili ya mumeo,kwani sauti ni silaha muhimu  huongeza nakshi katika masikio yake… usifanye hivyo mbele ya wanaume wengine ni haramu .

6. MTINDO

Jitahidi mara kwa mara kubadili mtindo wa nywele, manukato na kadhalika.

Lakini usizidishe kiwango na ufanye hivyo kwa mumeo tu.

7. MAHANJUMATI

Mpikie chakula kitamu ajirambe maana waliosema "the way to a man's heart is through his stomach" hawakukosea.
Ukiachilia mbali wale watu wachache wanaokula ili kushiba wengi huwa wanajali ladha tu.

Mpe mapishi matamu ili kumfanya akumiss pale anapokosa huduma yako.

8. SHUKURU

Kuwa mwenye shukrani kwa mumeo Kwa kikubwa na kidogo.  Ukiwa mwenye shukrani, mumeo atazidi kukupenda na atajitahidi kukufurahisha na kukuridhisha zaidi.

Ukiwa mtovu wa shukrani, mumeo atasikitishwa na hali hiyo na kuanza kujiuliza: “Kwa nini nimfanye mambo mazuri mtu asiyekuwa na shukrani?” Epuka Sana hali hiyo.

9. HESHIMA NA UTIIFU

Daima kuwa mtiifu kwa mumeo pia uwe mwaminifu kwa kipenzi chako.

10. Muunge mkono kupitia kazi yake, fedha yake au mali yake pindi inapohitajika. Japo hii wanawake wengi hushindwa kufanya hivyo.

11. MAAGIZO.

Fuata maagizo yake kama kufanya ibada, stara, ukarimu, nidhamu no. isipokuwa katika mambo ya haramu katika Uislamu.

mume ni kiongozi wa familia, na mke ni msaidizi na ni mshauri wake.

12. EPUKA

Jaribu kuepuka yale yanayomkasirisha mumeo

Mfurahishe anapokuwa ameghadhibika.

13. OMBA RADHI

Ukimkosea mumeo muombe msamaha. Na akikosea usihamaki kwa kumfokea au kuzozana naye.

Subiri anapokuwa hana ghadhabu na uzungumze naye kwa amani na kwa kauli nzuri.

14. MAPENZI MATAMU


Mpe mapenzi motomoto kwa style mbalimbali usiwe na style moja , usichelewe kumpa mahaba pindi mumeo anapojiwa na hisia ya kutaka kufanya mapenzi.

Mwambie maneno mataamu na yenye mvuto wa kimahaba.

15. MSIFIE MUMEO

Jua kumsifia babydady kwa zuri atakalokufanyia sio unakaa kimya.

16. ENJOY NAYE.

Mtoe out babydady siku moja moja na siku nyingine, pendelea kutumia muda mwingi kuongea nae maneno mazuri mkiwa wote nyumbani/chumbani.

17. MASSAGE.

Mfanyie massage ya mwili na sehemu nyeti mumeo, vilevile msinge mmeo anapokua nyumbani siku za weekend tumia muda mwingi kumfanyia hayo mambo.

18. MAJINA MATAMU.

Mwite mpenzi wako majina mazuri ya kimapenzi , haiji kumwita mumeo baba sikujua? khaaa, ina husu......

Ili kuiteka akili ya mwanaume muite majina mazuri kama honey, dear, sweet, darling, dady ukishindwa mwite jina lake nusu liwekee swagaa flan

 mfano waweza ita my Jey, badala ya jumaa au Bin Rash  wangu badala ya Bin Rashid wangu jitahidi best.

Best hakuna mchawi wa mapenzi ukifanya yote hayo utakua umeteka akili yake na hatobanduka kwako abadani..

Sunday, January 29, 2017

UKIFUATA MAMBO HAYA KUMI UTAKUA UMERAMBA SUMU YA PENZI NA HAUTOUMIZA/HUTOUMIZWA KAMWE…

UKIFUATA MAMBO HAYA KUMI UTAKUA UMERAMBA SUMU YA PENZI NA HAUTOUMIZA/HUTOUMIZWA KAMWE…



1. Wivu Wa Kupindukia
Ni Jambo Jema Kwa Mwanamume Kumtakia Heri Mpenzi Wake Na Kufanya Kila Awezalo Kuhakikisha Kuwa Hapati Madhara, Lakini Iwapo Utakuwa Mtu Wa Wasiwasi Na Mashaka Pale Unapomwona Mpenzi Wako Akizungumza Na Mwanamume Mwingine, Au Anapotoka Na Marafiki Zake Wa Kike, Au Anapovaa Nguo Inayomfanya Atamanishe, Basi Fahamu Kuwa Tayari Umekunywa Sumu Ya Mapenzi.

Katika Uhusiano Wa Kimapenzi, Kuaminiana Ni Jambo Muhimu Sana. Kama Kweli Unataka Mpenzi Wako Akupende Kwa Dhati, Mwoneshe Kuwa Unamwamini Na Unaheshimu Maamuzi Yake, Ikiwa Ni Pamoja Na Maamuzi Ya Kutoka Na Marafiki Zake Wa Kike Na Kuwa Na Marafiki Wa Kawaida Wa Kiume. Ondoa Hofu Na Acha Kabisa Kumpeleleza, Maana Wapo Wanaume Ambao Hutumia Muda Wao Mwingi Kuwapeleleza Wapenzi Wao Ikiwa Ni Pamoja Na Kuwategeshea Kamera Na Rekoda Za Simu.

2. Kutomwachia Nafasi Mpenzi
Kama Huishi Na Mpenzi Wako Ni Jambo La Kawaida Kuwa Na Hamu Ya Kumwona Mara Kwa Mara, Lakini Kumbuka Kuwa Mpenzi Wako Naye Ana Maisha Yake Na Anahitaji Nafasi Ya Kuwa Peke Yake Kwa Ajili Ya Mambo Yake Binafsi.

Hisia Za Kutaka Kuwa Na Mpenzi Wako Muda Wote Zinaweza Kudhaniwa Kuwa Ni Za Mapenzi Ya Dhati, Lakini Kwa Hakika Hiyo Si Ishara Njema Ya Mapenzi Ya Kudumu. Hebu Jiulize Kama Unaweza Kuendeleza Hali Hiyo Maisha Yako Yote. Ni Wazi Kuwa Utachoka. Kwa Hiyo, Mpe Mpenzi Wako Fursa Ya Kupumua. Namna Hii Mpenzi Wako Atajenga Hamu Ya Kutaka Kukutana Nawe Lakini Ukiwa Naye Muda Wote Hamu Hiyo Itaisha.

3. Kumwamulia Mpenzi Mambo Yake
Unaweza Kujikuta Ukisukumwa Kumwambia Mpenzi Wako Awe Anavaa Nini Wakati Gani, Akutane Na Nani Na Kwa Wakati Gani Au Ale Nini. Ukiona Hivyo, Fahamu Kuwa Hayo Si Mapenzi, Bali Umepitiliza Na Pengine Mwisho Wa Uhusiano Wenu Unanukia.

Hata Ukiachilia Mbali Suala Zima La Usawa Wa Jinsia, Hakuna Mwanamke Ambaye Angependa Apangiwe Kila Kitu Kuhusiana Na Maisha Yake. Kama Ilivyodokezwa Hapo Juu, Kila Mtu Ana Maisha Yake Na Kilichowaunganisha Ni Mapenzi Tu. Kama Utataka Kumpangia Kila Kitu Ni Wazi Kuwa Utaishia Kuishi Peke Yako.

4. Kumuuliza Mpenzi Maswali
Iwapo Utajikuta Ukimuuliza Mpenzi Wako Maswali Mengi Yanayoonesha Wasiwasi Wako Kuhusiana Na Mwenendo Wake, Fahamu Kuwa Kuna Tatizo Na Tatizo Hilo Lisipopatiwa Ufumbuzi Utakuwa Mwanzo Wa Mwisho Wa Uhusiano Wenu.

Mwanamke Angependa Umuulize Maswali Ya Kawaida Kuhusiana Na Jinsi Siku Yake Ilivyokuwa Na Kama Marafiki Zake Hawajambo Au La, Lakini Kila Jambo Lina Mpaka Wake. Mwanamke Hatarajii Kuwa Kila Mnapokutana Atakuwa Kama Ameingia Kwenye Chumba Cha Mtihani Au Usaili Wa Kazi.

5. Kutoamini Anachokweleza Mpenzi
Wakati Mwingine Watu Hushindwa Kuwaamini Wenzao, Lakini Kwa Sababu Ambazo Ni Za Msingi, Lakini Kuna Wakati Ambapo Mtu Hushindwa Kumwamini Mwenzake Bila Sababu Yoyote Ya Msingi, Au Kwa Sababu Zisizo Sahihi, Kisingizio Kikiwa Ni Mapenzi.

Kuna Tatizo La Kisaikolojia La Kujishuku Au Kuwashuku Wenzako. Hili Ni Jambo Ambalo Linaweza Kukuharibia Mustakabali Wako Katika Mapenzi, Maana Husababisha Kujengeka Kwa Mazingira Ya Kutokuaminiana. Ili Uweze Kwenda Sanjari Na Mpenzi Wako, Amini Kila Anachokweleza Hadi Pale Utakapokuwa Na Sababu Za Msingi Za Kutokumwamini. Na Hata Unapokuwa Umelithibitisha Jambo, Endelea Kuwa Katika Uhalisia Wako.







6. Kuacha Hobi, Marafiki
Mahusiano Ya Kimapenzi Mara Nyingi Huhusisha Kila Mmoja Kuacha Baadhi Ya Mambo Yake Kwa Ajili Ya Mwenzake. Hata Hivyo, Lengo Ni Kuweka Tu Uwiano Wa Mahitaji, Si Kuacha Kila Kitu Ulichokuwa Nacho Kwa Ajili Ya Mwenzako, Ama Kwa Shinikizo, Au Kwa Kulewa Penzi.

Iwapo Utabaini Kuwa Marafiki Zako Sasa Wamekuwa Ni Marafiki Zako Wa Zamani Na Hobi Zako Zimebaki Tu Katika Kumbukumbu Japo Kwa Hakika Bado Unahisi Mapenzi Katika Hobi Hizo, Basi Tambua Kuwa Huyo Mrembo Wako Amekunywesha Sumu Ya Penzi Na Sasa Huwezi Hata Kuitumia Vema Mantiki Yako.

Mbaya Zaidi, Iwapo Utabaini Kuwa Marafiki Zako Wapya Ni Marafiki Wa Siku Zote Wa Mpenzi Wako Na Hobi Zako Ni Zile Za Mpenzi Wako, Basi Tambua Kuwa Huna Tena Nafsi Yako, Bali Umejisalimisha Mzima Mzima Kwa Mpenzi Wako. Lakini Msemo Mmoja Wa Hekima Unatwambia Usiweke Mayai Yako Yote Kwenye Kikapu Kimoja. Yamkini Unaelewa.

7. Kukubali Kupelekeshwa
Pengine Unakumbuka Kuwa Kuna Nyakati Ambapo Ulikuwa Na Uwezo Wa Kujikita Katika Jambo Moja Na Kulifanya Kwa Umakini, Huku Ukiwa Pia Mwerevu, Mjanja Na Unayejisimamia, Lakini Leo Unayeyuka Kirahisi Tu Kama Barafu Iliyowekwa Juani! Hii Ni Hatari Kwa Mustakabali Wa Maisha Yako.

Mbaya Zaidi Ni Pale Utakapoiacha Kazi Yako Inayokulipa Vizuri Na Kufanya Kazi Nyingine Kwa Ajili Ya Kumfurahisha Mpenzi Wako. Ukifika Hali Hii Ujue Wewe Mwenyewe Kuwa Hapo Hakuna Mwanamume.

8. Utayari Wa Kufa Kwa Ajili Yake
Umewahi Kujisikia Kuwa Na Utayari Wa Kufa Kwa Ajili Ya Mpenzi Wako? Kama Jibu Ni “Ndiyo”, Basi Fahamu Kwa Hakika Kuwa Hayo Uliyo Nayo Si Mapenzi Bali Ni Upumbavu. Pengine Huku Ndiko Kunywesha Sumu Ya Mapenzi. Kwa Hakika, Hakuna Mwanamke Ambaye Anastahili Kumfanya Mwanamume Yeyote Kufa Kwa Ajili Yake.

Yamkini Wanaume Wanaolengwa Katika Makala Haya Si Wavulana Wanaosoma Sekondari, Waliobalehe Majuzi, Ambao Wakipenda Au Kupendwa Hujiona Kama Wako Katika Sayari Yao. Mwanamume Aliyepevuka Hujiamini Na Hayaweki Maisha Yake Yote Mikononi Mwa Mwanamke, Hata Kama Mwanamke Huyo Angekuwa Ndiye Mrembo Wa Dunia.

Iwapo, Ama Kwa Ujinga Au Kwa Kufahamu Umewahi Kumwambia Mpenzi Wako: “Ukiniacha Nitajiua,” Na Ukawa Unaamini Hivyo Kabisa, Basi Yamkini Unahitaji Kutafuta Msaada Wa Ushauri Nasaha, Maana Kwa Hakika Umepotoka.

9. Muda Wote Unawasiliana Naye
Vijana Wa Siku Hizi Ni Watumiaji Wazuri Sana Wa Simu, Lakini Iwapo Utabaini Kuwa Asilimia Kubwa Ya Muda Wako Unautumia Ama Kwa Kuongea Au Kuwasiliana Kwa Ujumbe Mfupi Na Mpenzi Wako, Basi Fahamu Kuwa Kuna Tatizo Ambalo Linahitaji Ufumbuzi Wa Haraka.

Kumbuka Kuwa Mapenzi Hayachukui Nafasi Ya Kila Kitu. Yamkini Huyo Mpenzi Wako Amekukuta Unaishi Na Kuna Mambo Ya Muhimu Ya Kufanya. Hebu Achana Na Simu Kwanza Ufanye Mambo Ya Muhimu Kuhusiana Na Maisha Yako. Kama Mpenzi Wako Hakwelewi Katika Hili Basi Hakufai.

10. Ndugu Zake Wanakufuatilia
Iwapo Utabaini Kuwa Marafiki, Ndugu Na Jamaa Za Mpenzi Wako Wanamtonya Mpenzi Wako Kuhusiana Na Kile Wanachokiita Mwenendo Wako Mbaya, Usipuuze Hali Hii. Kuna Uwezekano Mkubwa Kuwa Watu Hawa Wanayo Sababu Ya Kuwa Na Wasiwasi Na Mwenendo Wako, Kwa Hiyo Jichunguze Na Kuangalia Jinsi Unavyoenenda.

Hata Hivyo, Jambo Hili Si Ishara Njema Ya Mustakabali Mwema Wa Uhusiano Wenu. Iwapo Mpenzi Wako Ataweka Watu Wake Wakufuatilie, Maana Yake Halisi Ni Kwamba Hakuamini. Katika Hali Kama Hii, Haitarajiwi Kuwa Mustakabali Wa Uhusiano Wenu Utakuwa Mzuri, Kwani Kutakuwa Na Uingilizi Mwingi Wa Ndugu, Jamaa Na Marafiki Zake. Unaweza Kukubali Kuendelea Kuishi Katika Hali Hii Kwa Kisingizio Cha Mapenzi, Lakini Ukweli Ni Kwamba Hayatakuwa Mapenzi Bali Karaha.

KUWA MAKINI
Kama Unavyoona, Hizi Ni Baadhi Tu Ya Dalili Kuwa Mapenzi Yako Kwa Mwanamke Sasa Yanaelekea Katika Ulevi, Mithili Ya Ule Wa Dawa Za Kulevya. Jambo Moja La Kukumbuka Ni Kwamba Kweli Mapenzi Ni Kitu Kizuri, Lakini Pia Mapenzi Yanahitaji Kuwa Jambo Linaloashiria Mustakabali Mwema Kwa Wahusika Wawili. Yakiwapo Mambo Haya Kumi Hauwezi Kuwapo Mustakabali Mwema Katika Mapenzi.

Nacte imezitaja shule 10 bora kitaifa na shule 10 za mwisho kitaifa

[00:41, 1/28/2017] ‪+255 788 683 892‬: Mh Joyce Ndalichako atangaza rasmi siku ya matokeo ya kidato cha nne yaani NECTA "CSEE" ni siku ya tarehe 12/2/2017 kwa mwaka wa masomo na wanafunzi watakao faulu watalazimika kuingia shuleni siku ya tarehe 1/4/2017 wanafunzi hao wawe na pass 3 na spl pass 2 ili wajiunge na kidato cha tano kwa mwaka mpya wa masomo na wanafunzi, na kuzielezea skuli zilizofanya udanganyifu kwa upande wa Unguja ni K/SAMAKI, K/KWE "C", FARAJA, TUMEKUJA, na kuzitaja zilizofanya uzur pia hivyo kuhusu matoke ni mazur kwa asilimia 75% kuliko mwaka ulopita. HABARI HII IMETOLEWA KATIKA SHIRIKA LA UTANGAZAJI TBC.
[00:41, 1/28/2017] ‪+255 788 683 892‬: https://www.youtube.com/watch?v=Atx8Bo3xHDU&feature=youtube_gdata_player

Saturday, January 28, 2017

FAIDA ZA KULA MATANGO (CUCUCMBERS)KUTIBU MARADHI NA KUTUMIKA KWA UREMBO

FAIDA ZA KULA MATANGO (CUCUCMBERS)KUTIBU MARADHI NA KUTUMIKA KWA UREMBO

Tango ni tunda moja wapo yenye maji mengi kama vile tikiti maji ,linabeba virutubisho vingi vitamin K,B,C,potasium,manganese .Tango lina polyphenols ambayo inasaidia kukuepusha kupata maradhi sugu.Ni vizuri mkatumia matanga mara kwa mara kwa kutengeneza juice,kuchanganya kwenye kachumbali (salad)bila kumenya  maganda yake yanabeba virutubisho vizuri,au unaweza weka kwenye mkate na kuchanganya na maji ya kunywa kuyapa ladha na vitamins.



Umuhimu wa kula tango kwa afya yako



1.Kuipa kinga ubongo
Tango lina anti-inflammatory flavonol inayopelekea kuipa kinga ubongo na kukufanya kuwa na kumbukumbu nzuri (improve your memory).



2.Kupunguza hatari ya kupata cancer.
Tango linakupunguzia hatari ya kuapata cancer ya maziwa na shemu za uzazi (uterine,mayai ya uzazi (ovari).



3.Kutoa harufu mbaya mdomoni.
Kata kipande cha tango weka mdomoni kwa dakika 5 fanya mara 3 kwa siku inataidia kutoa bakteria wafanya kunuka mdomo .



4.Kupunguza stress.
Tango linavitamins B,vitaminB1 vitaminB5 na vitamini B7 ambazo zinakupunguza stress.



5.Kusaidia mmeng’enyo wa chakula.
Tango lina maji maji na fiber inayosaidia mmeng’enyo wa chakula tumboni,kwa wale wenye  tatizo la kupata haja kubwa(constipation) kula tango bila kumenya ganda lake, linabeba fiber itakayo kusaidia kuapa choo kwa urahisi.





6.Wenye matatizo ya moyo
Tatizo la pressure linaweza kupunguzwa kwa kula matango mara kwa mara sababu tango lina potasium inayofanya kushuka pressure kwa urahisi na salama.



7.Kupunguza  hatari ya kupata kisukari,kupunguza cholesterol8.Kutibu maumivu ya viungo9.Kufanya kuwa na ngozi laini na kukuza nywele kwa haraka.







11.Kutumika kutoa alama nyeusi chini ya macho.
Kata tango umbo la duara weka kipande kimoja kwa kila jicho, fanga macho ndio uweke kwa juu . Kwa matumizi ya uso(facial ) pia unasaga iwe laini (puree) na paka usoni acha kwa dakika 20 ,kish nawa kwa maji safi itakufanya kuwa soft na fresh.

12.Kutoa sumu mwilini.
tengeneza juice ya tango,unaweza changanya na apple,spinachi na limao saga pamoja ni njia nzuri ya kutoa sumu mwilini kwa wale wanaotumia madawa kali n.k

Friday, January 27, 2017

MAMBO 10 YANAWEZA KUWA KAMA KICHOCHEO CHA USALITI KATIKA NDOA AMBAYO HASA NI TATIZO LA MOYO

MAMBO 10 YANAWEZA KUWA KAMA KICHOCHEO CHA USALITI KATIKA NDOA AMBAYO HASA NI TATIZO LA MOYO.

1. Kutokuvutia tena
• Moja ya sababu iliyopelekea kukubali kuoa au kuolewa na huyo mwenzi wako, kuna baadhi ya vitu ulivutiwa navyo ndio akawaacha woote na kumchagua huyo.
• Vitu hivyo usipovizingatia na kuvi “maintain” vitasababisha hali ya kukinai kwa mwenzi wako na mwisho kuanza kuvutiwa na wengine kule nje.

2. Kutokujali tena kuwa unaongezeka unene, kubadilika unavyoonekana na 
• Kila mwanandoa ana “test” yake ya mvuto kwa mwenzi wake.
• Kuna mwingine alikupenda kwasababu ya wembamba wako sasa unapojiachia na kuwa mnene ila hamu ya kuendelea kuvutiwa nawe inapungua na baadaye inakwisha na kusababisha aanze kuchungulia nje ya “fance”

• Kuna mwingine alikupenda kwasababu ya unene au kujazia katika maeneo Fulani Fulani. Sasa mwili ukiporomoka unapoteza ule mvuto tena na kumfanya apoteze hamu ya kuwa na wewe na kumfanya kuanza kuchungulia chungulia nje.

• Ni vizuri kujali afya yako na kujua ni vitu gani vinavyomvutia mwenzi wako kutoka kwenye mwili wako na ujitahiti kuvitunza “maintain” ili kuendelea kudumisha ule mvuto kwa mwenzi wako.

3. Kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa.
• Tendo la ndoa ndio mhimili unaoishikilia ndoa.
• Ukiona hamu ya tendo la ndoa imepungua kwa mwenzi wako ujue majanga yanakunyemelea.
• Kufanya tendo la ndoa mara chache miongoni mwa wanandoa ni ufa wa kubomoa ukuta na ulinzi wa ndoa.

• Muda si mrefu utaanza kutamani wengine na mwisho wake utaangukia huko.

4. Kukosa hamu katika mavazi mazuri kwa ujumla, mtindo wa nywele na jinsi unavyoonekana. 
• Hili hasa ni kwa wanawake. Kable ya kuolewa ulikuwa unajitahidi sana kujipemba na kujitunza kila wakati ulikuwa safi na nadhifu.
• Pochi yako ilikuwa haikosi vi pafyumu pafyumu. Sasa umesahau hata bei za pafyumu zinauzwaje.
• Sasa umeolewa, unashinda na upande wa kanga au kitenge kifuani toka asubuhi mpaka jioni wala huna habari.
• Mumeo kila akikuangalia mpaka haamini kama ni wewe aliyekuoa ukiwa mrembo na wa kuvutia.
• Unavaa nguo nzuri tu pale tu unapotoka kwenda kanisani au mtoko maalumu.

5. Kukosekana kwa mawasiliano
• Mawasiliano yanaushisha pande zote mbili.
• Anayetoa na anayepokea

6. Kushindwa kuendeleza yale yanayompendeza kila mmoja wenu.
• Mnakubaliana mipango kama wanandoa lakini utakelezaji unakua mgumu.
• Mmoja anakuwa tayari kutekeleza na mwingine anashindwa.
• Aliyetayari kutekeleza anavunjwa moya sana na Yule ambaye sio mtekelezaji.

7. Ndoa za kipindi cha likizo. 
• Wanandoa wanaonana siku kumi na nne tu kasha kila mtu anasafiri kurudi anakofanya kazi.
• Wapo baadhi ya wanandoa kutokana na mazingira yao ya kazi wanaonana kila baada ya miezi 6 au wengine hata mara moja kwa mwaka.
• Hii hasa ni kwa wanandoa wanaofanya kazi mikoa mbali mabili au nchi mbalimbali.
• Wanatafuta pesa wakiua ndoa zao kwajili ya kusaka pesa.
• Ni heri kuacha kazi hiyo na kuishi maisha ya kawaida kuliko kuwa na ndoa kama hii.
• Kiufupi hii sio ndoa.

8. Kushindwa kushirikiana chumba cha kulala.
• Zipo baadhi ya ndoa mume analala chumba chake na mke analala chumba chake.
• Wapo wanandoa pia ambao wanalala chumba kimoja ila vitanda tofauti
• Kuna wengine wanalala chumba kimoja ila mmoja analala kitandani na mwingine analala chini.

9. Kushindwa kumfikisha mwenza wako mara kwa mara katika tendo la ndoa.
• Sio swala la kushiriki tu.
• Mnaweza mkawa mnashiriki lakini je ushirika huo unamridhisha kila mmoja wenu?
• Mmoja anapokuwa anapunjika kila siku anakula lakini hashibi, inafungua mlango wa kumtafuta mshibishaji mwingine ili aweze kumshibisha.
• Tatizo hili ni kubwa sana hasa kwa siku za leo.
• Wanaume wengi ni wavivu na wenye ubinafsi.
• Wanalishwa vizuri ila wanajishibisha wenyewe tu na kuwaacha wake zao wakiishi kwa njaa ya muda mrefu na matokeo yake michepuko imekuwa ikiongezeka kila iitwapo leo.

10. Kufanya kazi pamoja mwanamke na mwaname asiye mwenzi wako kwa muda mrefu.
• Sumaku na bati vikikaa karibu mwishowe vitanasa.
• Mwanamke na mwanaume wanaofanya kazi pamoja kwa muda mrefu wakiwa katika mazingira ya private huishia katika kutamaniana.
• Kazi za kusafiri kwa pamoja mwanamke na mwanaume na kukaa hotel moja kikazi wakiwa wawili tu huweza kuongeza kazi ya ziada ambayo ni sumu kwa ndoa zao.
• Kwenda kusoma pamoja kozi za nje kati ya wawili hao, wanaweza kuvumila sikuchache za kwanza na baada ya hapo huweza kujikuta wakiwa katika ukurasa mwingine.
• Kwenda safari mbali za kikazi pamoja umakini usipozingatiwa ni majanga.
• Kufanya vikao katika vyumba vya hotel mwanamke na mwanaume.
• Kujifungia kufanya counselling au maombezi mwanamke na mwanaume wawili tu chumbani ni majanga.
• Kujifungia chumbani mwanaume na mwanamke wawili tu kusoma na kubukua kwajili ya mtihani ni majanga


BORESHA AFYA YA NYWELE ZAKO KWA KUTUMIA TUI LA NAZI


BORESHA AFYA YA NYWELE ZAKO KWA KUTUMIA TUI LA NAZI


Wanawake wengi wamekuwa wakihangaika katika kuhakikisha kuwa wanatunza nywele zao dhidi ya matatizo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa na mba au kukatika kwa nywele jambo ambalo limekuwa likiwagharimu pesa pia.



Wataalam wa tiba za asili  wanasema kuwa njia mojawapo ya kuboresha nywele zako ni kuziosha nywele kwa tui la nazi, ambapo anasema kuwa mara baada ya kuosha nywele zako vizuri, ukachukuwa tui la nazi lililochunjwa vizuri na uoshee nywele zako huku ukihakikisha tui hilo linafika hadi kwenye vishina vya nywele.


Wataalam hao anaendelea kubainisha kuwa tui hilo litakuwa ni tiba nzuri kwa ajili ya tatizo la mba na kuzifanya nywele zako kukua kwa haraka zaidi na kuzifanya zionekane zenye afya tele.


Mbali na mafuta hayo ya nazi, wa taalamu wanashauri, kuwa mbegu za ndimu na pilipili manga zikichanganywa pamoja na kupondwapondwa na kisha kuchanganywa na tangawizi, mchanganyiko huo husaidia sana kuotesha nywele endapo mhusika atapaka kila siku jioni.





Vitu vingine ambavyo vinaweza kurutubisha nywele zako ni pamoja na ndimu, ufuta na mafuta ya nazi



Thursday, January 26, 2017

DALILI KUMI NA TANO ZA MAPENZI KUNYAUKA



DALILI KUMI NA TANO ZA MAPENZI KUNYAUKA


Wapenzi wengi ambao wamefikia hatua ya kuachana wameshindwa katika vipimo vya kitalaamu kuthibitisha ubaya waliokoseana, ambao unaweza kubeba uamuzi huo mzito wa kuvunja ahadi zao za kimapenzi na hata ndoa.

Kwa mujibu wa watalaam wa masuala ya ndoa na mapenzi inaelezwa kwamba wapenzi wanaoachana huwa hawana sababu za msingi, hii inatokana na ukweli kwamba wanaoachana hawafahamu kiini kilichowatenganisha katika makubaliano muhimu na ya kwanza kabisa ulimwengu ya watu kufikia hatua ya kupeana utu wao.

Inasemwa hivyo kwa sababu ukilinganisha matatizo yanayotenganisha watu hayabebi hoja zinazokubalika na wapenzi wote. Kwa mfano kama wapenzi watasema wameachana kwa sababu wamefunaniana na wakadhani hiyo ni sababu wanakuwa wanaudanganya zaidi umma kwa maana kuna wanaofumaniana, wanaodhalilishana, wanaotukanana, wasioheshimiana kabisa, lakini bado wanadumu katika ndoa zao bila kuachana.

Kwa ulinganifu huo, wachunguzi wa mambo ya ndoa wanasema, kuachana si zao linaloota na kukua kwa siku moja, bali ni migogoro isiyoshughulikiwa kwa muda mrefu ambayo huwaachanisha wanandoa taratibu bila wao kujua.

Kwa maana hiyo wanaoachana au watakaoachana wanatakiwa kufahamu kuwa safari yao ya talaka haianzi na kumalizika kwa siku moja, isipokuwa hufikia katika hitimisho baada ya kuwepo katika mwendo kwa muda mrefu, ambapo dalili zake huwa hizi zifuatazo:

1 : Ikiwa mmeoana na baadaye mkaanza kuonana ni watu msiohitajiana sana katika maisha. (mapenzi kuchuja). Kila mtu anafahamu kuwa wakati wa uchumba mapenzi huwa moto moto lakini baada ya kuoana hujitokeza hali ya kuanza kuzoea. Hii inatokana na ukaribu ambao mwanzo haukuwepo au kusitishwa kwa machimbezo yaliyokuwa yakiboresha uhusiano. Kwa mfano wapenzi wengi wanapokuwa kwenye uchumba hufanyiana mambo mengi yakiwemo ya kutumiana zawadi na kadi au kutoka pamoja kwa matembezi, lakini wakioana hujikuta hawafanyiani hayo, jambo ambalo huathiri mapenzi yao.

Uchuchuzi unaonyesha kuwa wapenzi walio kwenye uchumba wanapokuwa pamoja hutumia muda mwingi sana kuomngea kwa simu, kutumiana meseji, kuzungumza tofauti na mume na mke. Ukitaka kuthibitisha keti barabarani ukiona mwanaume na mwanamke wamo ndani ya gari hawaishi kucheka na kuzungumza wafuatilie utakuta mwisho wa safari yao wanaagana kila mmoja anakwenda kwake (ina maana si mume na mke hao). Ni nadra sana kuwakuta wanaume wakiwa pamoja na familia zao wakifurahi, jambo ambalo hupunguza upendo na kuleta mazoea na hisia za kutohitajiana sana. Hili halifai likiwepo ni ishara kuwa mapenzi yanakaribia kunyauka.


2 : Mkiwa hamsameheani na kusahau mnapokoseana. Si watu wengi ambao wako tayari kusamehe na kusahau makosa. Wapenzi wa dunia ya leo wakisema nimekusamehe haina maana wamefuta kosa bali hiliweka kando na kulikumbushia wakati mwingine. ‘Hili ni kosa la tatu tarehe fulani ulinifanyia hivi, wiki iliyopita na jana kulinijibu hivi hivi sasa leo siwezi kukuvumilia”
Kauli kama hizi hutoka kwenye vivywa wa watu ambao hawako tayari kusamehe, kosa la mwaka juzi litakumbushwa tena na tena na kuzidi kuchochea ugomvi hata uliokuwa mdogo na kuoneka mkubwa kwa sababu tu umehusishwa na makosa yaliyopita. Inashauriwa kuwa uhai wa mapenzi lazima uambatana na kusameheana kama wanadamu na kusahau makosa. Hili lisipofanyika ni rahisi kuua penzi na kuwafanya watu kuachana. Ni vema kila mmoja wetu akajichunguza tabia yake na kuacha kukumbusha makosa yaliyopita.


3 : Msipokubali kuwekeana mipaka ya kiutawala. Kuna suala linatambulishwa sana siku hizi na wanaharakati, linaitwa usawa wa kijinsia, jambo hili limekuwa likichangia sana migogoro ya ndoa hasa baada ya kutumiwa vibaya na wahusika. Hakuna ubishi mila za kiafrika zinaongozwa na mfumo dume, kuubadili mfumo huu kwa haraka kumekuwa kukiharibu uhusiano mwingi wa kimapenzi kutokana na ukweli kwamba ni wanaume wachache sana ambo wako tayari kuishi na wanawake wanaovutana nao kimamlaka.

Hivyo ili kunusuru hili lisiwe kikwazo katika mapenzi tunashauri kila mwanandoa kuheshimu mipaka yake na kujali zaidi utu na si usawa kama inavyotambulishwa (haya ni mawazo yangu). Watu wanaojali utu katika familia watakuwa tayari kuwapa heshima wanaoishi nao kwa kusikiliza mawazo yao na kutokutumia nguvu kuwakandamiza wengine. Ni vema mwanamke akachungua nafasi yake kwa mumewe na mume naye akamuheshimu mke kwa utu wake.


4 : Msipozungumzia vikwazo vya maisha.

Matarajio ya watu wengi wanapokuingia katika uhusiano wa kimapenzi huwa ni kupata faraja, ni wachache kati yao hufikiria kukutana na vikwazo vya kimaisha. Tafiti zinaonyesha kuwa wakati mtu anapotafuta mpenzi huamini toka moyoni kuwa akiwa na waridi wake matatizo ya upweke, kukosa msaada wa hili na lile yatakwisha lakini baadaye anakuja kubaini kuwa aliyokusudia kuyapata hayapati tena na hivyo kujuta kwa kauli kama hizi. “Kama ningejua kama mwanaume mwenyewe yuko hivi nisingekubali kuolewa.”

Kauli kama hizi mara nyingi hutokea kwa watu ambao hawazungumzii matatizo na vikwazo wanavyokutana navyo katika mapenzi na kuviondoa. Kama mpenzi wako ana matatizo unasubiri nini kuyatafutia ufumbuzi au kama maisha hayaendi sawa ukimya wa nini kwa mwenza wako, kaeni chini muambizane kuwa mnaupungufu wa fedha na dhiki kadhaa wa kadhaa, ili kama kutatokea kukosa mahitaji muhimu liwe ni jambo linaloeleweka na wote kuwa linatokana na kipato kushuka. Uchunguzi unaonyesha kuwa wanaume wengi wanapokukwama kiuchumi hupunguza matumizi kimya kimya jambo ambalo huwafanya wanawake wengi kubaki wakitumikia zana potofu kuwa huenda wananyimwa baada ya kuwepo kwa nyumba ndogo.

5 : Msipokuwa na mipango ya pamoja na uwazi wa matumizi ya pesa.

Nina ushahidi wa kutosha juu ya kuwepo kwa wapenzi hasa wenye kipato kutokuwa wawazi katika mipango yao ya kimaisha na matumizi yao pesa. Natambua baada ya kufanya uchunguzi wangu kuwa pesa za baadhi ya wanawake huwa hazina matumizi ya wazi, badala yake wanaume hubanwa kwa kisingizio kuwa wao ndiyo wana wajibu wa kutunza familia.
Hali hii imekuwa ikileta migogoro mingi sana kwenye familia na kushusha upendo kwa vile upande unaohudumia familia hapa haijalishi mume au mke huwa unajikuta ukikereka kwa kukosa msaada wa upande wa pili na hivyo kuondoa mapenzi ya kweli. Kama hilo halitoshi vijana wengi wa kiume siku hizi wamejikuta wakiahirisha mapenzi yao kwa wasichana baada ya kukosa ushirikiano wa kimapato na matumizi yake.

“Ninashida ya kuonana na wewe mpenzi wangu, vipi nikufuate kazini?” Jibu linakuwa “Hapana niko bize sana leo.” Inawezekana kabisa mtu akawa hayuko bize lakini kwa sababu anaogopa kukamuliwa kipato na yeye mambo yake hayako sawa anaamua kukacha ahadi. Lakini ukiwepo ushirikiano wa kimatumizi husaidia kudumisha mapenzi.
Inashauriwa kwamba kama wapenzi wote wana kazi na wanapokea mishahara ni vema vipato vyao vyote vikatumika katika kutunza na kuendeleza familia. Tabia ya mwanamke kumtegemea mwanamume kimatumizi huku yeye akitumia pesa zake kwa manunuzi ya vipodozi na nguo au kufanyia mambo yake kwa siri haijengi badala yake inanyausha mapenzi kama siyo kuyaua kabisa.

6 : Mkiacha kujaliana na kupeana haki katika tendo la ndoa.

Tendo la ndoa ni muhimu kwa wanandoa kwa vile linahusika na hizia za mwili. Matatizo mengi ya usaliti kwa mujibu wa uchunguzi, yanatokana na wapenzi kutotoshelezana wakati wa tendo la ndoa. Kwa kutokutambua madhara au kwa uzembe, wapenzi wengi wamekuwa wakiacha kutimiziana tendo hilo bila kuwepo kwa sababu za msingi. “Mimi nimechoka siwezi kufanya mapenzi.”
Inawezekana kweli mtu akawa kachoka sawa na kauli hiyo lakini sababu hiyo haiwezi kumfanya mwenza akazimaliza hisia zake, isipokuwa kwa kutafuta njia mbadala zikiwepo za usaliti. Sambamba na hilo wapenzi wengi wamenyausha mapenzi yao kwa kutokuwa wabunifu katika uwanja wa sita kwa sita kwa kutokujituma, kutobuni staili mpya, kutochombeza na kutohamasisha kwa cho chote na kibaya zaidi kutokuwepo kwa usafi wa mwili yao.

Katika kipindi cha maisha yangu ya ushauri wa masuala ya saikolojia, maisha na mapenzi nimekuwa nikikutana na wanaume wengi wanaolalamika kuwa wana upungufu wa nguvu kiume. Lakini wengi kati ya hao ambao mamia yao nimeshawasaidia walijikuta wakipungukiwa nguvu zao kwa sababu za kisaikolojia zilizochochewa pia na udhaifu wa wenza wao. Kama utakuwa na mtu kwa mfano, ambaye mtakutana naye chumba kile kile, eneo lile lile, staili zile zile, kwa miaka mitano mfululizo bila shaka hali ya kukinaishwa itakuwepo na hivyo mapenzi kunyauka. Katika hili ni vema kujifunza zaidi namna ya kutoshelezana katika tendo la ndoa.

7 : Mkibeba fikra binafsi kwa kila mtu kutaka mafanikio yake.

Maisha ya wapenzi wengi yamekuwa yakipoteza maana kiasi cha kufikia kuchuja kutokana na wapenzi wenyewe kuwa na mawazo ya ubinafsi. Utakuta watu wameoana lakini kila mmoja anakabili changamoto za maisha peke yake, hali ambayo humfanya atumie nguvu kubwa kutafuta ushindi wa matatizo yake.

Mantiki ya maisha ya ndoa ni kusaidiana. ‘Mungu alimwambia Adamu kuwa atampatia msaidia wa kufanana naye ambaye ni mwanamke aliyeitwa Hawa.’ Upo pia msemo usemao ‘Kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi’ Ni wajibu wa wanandoa kuhakikisha kuwa maisha yao yanakuwa ya nyuzi mbili ili yasikatike upesi. Lakini ikiwa kila mtu anajenga nyumba yake, anafanya biashara zake, ana mipango yake binafsi ujue mwisho mbaya wa mapenzi umesogea.

8 : Mkiwa watu wa kutoa siri zenu nje.

Upo udanyanyifu mwingi wa kimawazo miongozni mwa wapenzi wengi kiasi cha kudhani kuwa kumwambia rafiki au ‘shoga’ masuala ya ndani ya ndoa ni kutafuta suluhu ya matatizo. Hii si sahihi kwa vile upo ushahidi mkubwa juu ya wapenzi wengi ambao walijikuta katika wakati mgumu baada ya kutoa siri zao nje. Ifahamike kuwa ndoa imara ni ile inayoheshimika katika jamii, na heshima hiyo haiwezi kuwepo kama wanandoa hawatakuwa makini katika kutunza siri za mapenzi yao.

Haipendezi kwa mwanamke/ mwanaume kwenda kijiweni na kuanza kuanika mambo ya ndani kwa mfano. ‘Yaani leo mume wangu hakuacha kitu chochote ndani sijui itakuwaje. ‘Sema wanawake wote lakini si mke wangu, ana kasoro nyingi sana.’
Kauli kama hizi na nyingine ambazo zinatoa nje udhaifu wa maisha yenu hazifai, kwani katika kila ndoa kuna udhaifu mwingi ukiwepo ukimya ina maana wahusika wanaweka udhaifu wao kifuani kwa maslahi ya maisha yao. Na wewe uwe hivyo kwa kutunza siri za mumeo.mkeo.

9 : Msipokuwa wawazi katika kuzungumzia upungufu wa kibinadamu mlionao na kusaidiana.

Wapenzi wasomaji wangu, hakuna mwanadamu aliyekamili kwa asilimia mia moja. Ukimuona hodari wa hili ni dhaifu wa lile, kinachotakiwa ni kusaidiana katika kufikia ukamilifu. Faraja inayopatikana katika upungufu wa mwanadamu hasa usiokuwa wa kimaumbile ni kuwepo kwa utatuzi wake. Kuna wapenzi wengi wamefikia kuachana kwa kasoro ndogo ndogo kama za kutojua mapenzi, au hata uchafu wa mwili ambao kama wangekaa na kujadiliana pamoja wangepata ufumbuzi wa tatizo.

Inashauriwa kuwa kunapokuwepo upungufu wowote wa kati ya mwanaume na mwanamke ni wajibu wa wapenzi wenyewe kukaa chini na kuelezana wazi na kushirikiana katika kupata ufumbuzi. Unashindwa nini kuwambia mpenzi wako kuwa hakutoshelezi katika tendo la ndoa, ana harufu mbaya mwilini, mchafu, hajui mapenzi na mambo kama hayo! Kikubwa katika hili ni kujua namna ya kuwasil;isha ujumbe, maana kuna wengine hawana lugha nzuri za mawasiliano “Yaani mke wangu unanuka sana mimi nakerwa sana” Ukisema hivi utamfanya mwenzako aone kama unamnyanyapaa. Tumia lugha nyepesi itakayosaidia kumaliza tatizo msikae kimya bila kuzungumzia upungufu wenu mtajikuta mnaachana.

10 : Mkiendekeza nguvu katika kutwaa madaraka ndani ya familia.

Kuna baadhi ya familia kila mmoja ni mtemi hakuna diplomasia katika kutatua migogoro. Utakuta mwanamke ni mbogo na mwanaume naye ni simba, basi shughuli inakuwa nzito. Ndoa inakuwa uwanja wa ndodi kila siku kutoana manundo. Hakuna mapenzi ya namna hiyo! Kanuni za mapenzi bora zinakataza wapenzi kutumia nguvu kutwaa madaraka au haki ndani ya familia. Inawezekana kabisa wewe kama mke/ mume ukwa na haki katika jambo fulani lakini haki hiyo haikupi fursa ya kutumia nguvu nguvu kuipata.

Kinachotakiwa katika mapenzi ni kuheshimiana, kwani katika hali ya kawaida utumiaji wa nguvu katika kudai haki ndani ya familia ni moja kati ya mambo yaliyoshindwa katika historia kuleta maelewano. Kama unadhani naongopa keti chini ujitathmini tangu umeanza kumchunga mumeo/mkeo na kumbana kwa ngumi umepata mafanikio gani, ameacha tabia yake au ndo anazidi? Umwamba haufai kutumika katika maisha ya ndoa kwa mtu yoyote awe mwanaume au mwanamke.

11 : Mkiwa watu msioheshimiana mbele za watu na kupenda zaidi kusema kuliko kusikiliza.

Nimeshuhudia wapenzi wengi ambao hawajui umuhimu wa kuheshimiana mbele za watu. Utakuta mwanamke/mwanaume akimwaibisha mwenzake mbele za watu kwa kumfokea, kumwita jina baya, kumtusi, kumtoa kasoro na hata kumdhalilisha. Kitendo hiki ni kibaya na maumivu yake hudumu kwa muda mrefu akilini mwa mtendewa.
Inashauriwa kwamba wapenzi wanapokuwa mbele za watu wachunge ndimi zao na wawe watu wanaopenda zaidi kusikiliza kuliko kunena. Inaelezwa, penye wingi wa maneno yapakosi kuwa na uovu. Kuna wanawake wakianza kuwatusi waume zao mpaka nyumba ya 50 wanasikia au wakati mwingine hutoka nje na kumwaga mitusi kana kwamba wameambiwa watapewa tuzo. Hiyo si heshima na hajawahi mtu kuheshimika kwenye jamii kwa uhodari wa kutukana watu.


12 : Msipokuwa tayari kukubali kosa na kujirekebisha.

Dalili nyingine ya mapenzi kunyauka ni kwa wapenzi wenyewe kuwa na tabia ya kutokukubali makosa na kujirekebisha. Utakuta mwanaume/,mwanamke ameshaambiwa mara nyingi na mwenza wake juu ya tabia zake na pengine hata marafiki zake wamemtahadharisha lakini habadiliki, kila siku anarudia makosa yale yale ambayo yanamuumiza mpenzi wake. Huu ni mwenendo mbaya, ubinadamu unamtaka kila mtu kuwa tayari kukiri kosa na kujirekebisa

13 : Msipokuwa watu wa kuitafuta furaha pale inapokosekana.

Wakati mwingine harakati za maisha huleta huzuni, kwa mfano, kama wanandoa watafiwa, kuuguza, kufukuzwa kazi, kupoteza mali kwa kuibiwa na matukio kama hayo huondoa furaha. Hapa inashauriliwa kwamba endapo furaha itaondoka kwa sababu yoyote wanandoa wanajukumu la kuitafuta. Hapa namaanisha kutiana moyo na kuwezeshana kusonga mbele wakiamini kuwa hakuna marefu yasiyokuwa na ncha. Kuacha huzuni itawale nyumba yenu kwa muda mrefu hupunguza mapenzi.

14 : Msipozingatia kuombana msamaha bila kujali nani mwenye kosa.

Kuombana msamaha ni jambo la lazima kabisa katika ndoa, na busara inamtaka mwenza kuwa tayari kuomba masamaha hata kama anaona kabisa hakuna kosa la msingi alilolifanya mbele ya mwenzake. Kung’ang’ania kutaka haki kipindi cha kuzozana ni njia ya kuelekea kukosana zaidi na hatimaye kuachana. “Nakuomba unisamehe mke/mume wangu, najua nimekuudhi.” Baada ya kutoa kauli hiyo na mzozo kupoa mhusika anaweza kufafanua kilichotokea na hapo anaweza kueleweka zaidi kuliko kipindi ambacho mpenzi wake anakuwa na hasira.

15: Msipokuwa tayari kukumbushana wajibu na mwenendo wenu

“Atajijua mwenyewe siku yakimkuta ya kumkuta huko ndo atafahamu” “Mimi nimechoka nimebaki namwangalia tu.” Kubaki unamwangalia mpenzi wako anaharibikiwa si uamuzi wa busara kwani mwisho wa siku kama ni aibu itakufikia na wewe pia. Ukimuona mwenzako anakwenda nje ya mstari wa jamii mrejeshe na kuzidi kumkumbusha kila siku wajibu wake kama baba au mama wa familia, hii inasaidia kumuweka sawa mahali anapokosea.


Mpaka hapa tutakuwa tumefikia tamati ya somo letu, naamini watu wengi wamejifunza vya kutosha. Shukrani za pekee ziwaendee watu wote waliokuwa pamoja nami tangu mwanzo wa somo hili

Sababu 10 zivunjazo ndoa nyingi... Vijana na Wanandoa soma hapaa....

Sababu 10 zivunjazo ndoa nyingi... Vijana na Wanandoa soma hapaa....


Upendo
 Upendo wa kweli ni jambo muhimu sana katika maisha ya ndoa, vijana wengi hukimbilia ndoa kisa mali hasa vijana wa kike, bila kusahau ndoa ni pingu za maisha na huyo mtu utakaa nae milele. Upendo wa kweli usipokuwepo katika ndoa hii ndoa haiita dumu maana amani haita kuwepo pia faraja kati ka wanandoa haitopatikana na hio ndoa kugeuka maigizo.



Uwaminifu
Kama upendo wa kweli ukiwepo ndani ya nyumba, uaminifu hasa ndio waaitajika, kama hamta aminiana vitu vidogo tu vitawatenganisha, maana jamii kawaida huonea wivu ndoa na kutupa mishale ya maneno na matendo ili kuijeruhi ndoa yenu, na siri za ndani ni zenu kama wana ndoa sio za wote, na kama uaminifu hauta kuwepo ndoa itakaa kwa mashaka, na ndoa ya mashaka haidumu.


Msamaha
Kuna msemo wa kiingereza unasema “no body is perfect” kiswahili inamaana kuwa, “hakuna alie msafi” hii inamaanisha kuwa binadamu hukosema na anahitajika kusamehewa,kama ndoa haita weka msamaha kama ngao yao, muhimili wa ndoa hii uko matatani.

Uvumilivu
 Ndoa imeundwa na watu wawili ambao walitoka nyumba tofauti na maisha tofauti kabisa, ndoa huwajumlisha kutokana na tofauti zao, kabla ya ndoa kuna kitu kinachoitwa courtship(Uchumba) hiki ni kipindi ambacho wapenzi hujuliana tabia zao na kuunganisha tofauti zao na kawaida hutumia mwaka 1 mpaka 4 na ikizidi hapo ni tatizo, kukiruka au kukizidisha hiko kipindi huaribu ndoa nyingi sana na kama hapakuwa na maelewano ya tabia hapa mnaruhusiwa kuachana na kama ukilazimisa hiyo ndoa haitadumu.


Mawazo mgando
Katika ndoa wanawake wengi huwategemea wanaume katika kutafuta, na hata wengine wakijiita ni wanawake wa nyumbani, pia kuna wanaume wanao lelewa, ndoa haiwezi endelea kama hapatakuwa na maendeleo maana mwaweza pata watoto na kipato toka uchumba hadi mna watoto watatu ni kile kile mwisho wa siku ndoa huvunjika kisa kipato shida, mwanandoa kutumia njia mbadala(wizi, uzinzi n.k), kwa mwanamke epuka kuwa mke wanyumbani na mwanaume atafute kazi, hii pia husaidia katika tendo maana wote mnakuwa mmechoka tendo mnafanya kutafuta usingizi, vinginevyo ndio mchepuko unapoanzia.


 Mazoea
Mke ndio mpishi wa chakula cha ndoa, hata katika mapishi ya kawaida chakula huwa kina badilishwa tokana na ratiba au mpishi atavyojisikia, chakula cha ndoa kinaitaji maandalizi sawa na chakula cha tumbo, namaanisha kuwa mke na mume wanahitaji kujiandaa na kama hawatajiandaa hata  dakika 1 mwanaume hatafika yaani ataonja tu chakula cha ndoa na kulala, hii ni sawa na maisha ya kawaida ya nyumbani, nyumba inatakiwa iwe safi na ibadilishwe mipango kuondoa mazoea, pia chakula kinahitaji kubadilika sio sikukuu tu, na  wapenzi wabadilike hata pawe na out.


Kutotambua wajibu
Katika jamii yetu tumelelewa tukitambua wajibu wetu kwa kila jinsia tokana malezi na tamaduni, mwanaume alete chakula mezani  na mwanamke apike, lakini maisha yana badilika na sio kila siku sawa, mfano mke anamimba na vyombo havijaoshwa na nguo hazijafuliwa mwanaume akijitolea sio mbaya , tutambue wajibu wetu ili pande fulani isilalamike maana pakitokea malalamiko ndio mwanzo wa ndoa kuvunjika.


Utii
Tukishatambua wajibu wetu na utii hufuata, hili ni jambo muhimu katika ndoa, kama utii haupo ndoa na hata familia yote inaweza tengana, usemapo utii tunaanzia kutoka kwa mtoto mpaka kwa kichwa cha familia.


Uchafu
Hili ni tatizo kubwa sana ambalo huwezwa kufichwa katika kipindi cha uchumba, ila ni shida kulificha katika kipindi cha ndoa maana mko mwili mmoja, usafi unaoitajika ni wa mwili na roho, mwili unahusisha kuoga, kunawa miguu kabla ya kulala, sehemu za ndani za siri, harufu za makwapa, nakadhalika.Usafi uzingatiwe katika ndoa na wanandoa wajaribu kufanya usafi kuwa sehemu ya maisha yao maana kuna msemo usemao, “Ishi uongo mpaka uongo uwe maisha yako”.



Kusahau uwepo wa mungu
Uwepo wa Mungu katika ndoa hulinda tabia za wanadoa, ulinzi huu hufuatana na vitabu vya dini, ambavyo kazi zao ni kulinda maadili katika jamii, kusahau uwepo wa Mungu katika jamii huleta maovu ambayo husababisha mafarakano katika ndoa na hata kuvunjika kwake.


JE WAJUA PARACHICHI NI TIBA

JE WAJUA PARACHICHI NI TIBA YA CHUNUSI NA PIA HUIWEKA NGOZI YAKO IWE KAVU NA NYORORO





Parachichi ni tunda kama walivyozoea watu wengi,lakini linaweza kukuondolea tatizo la ngozi kukauka na kukuifanya iwe nyororo na ya kupendeza zaidi?
Kama bado ngoja leo nikujuze kuwa tunda hili ni moja kati ya matunda muhimu ambayo unaweza kuyatumia ukiwa nyumbani kutengeneza “homemade facial masks” kwa ajili ya uso


Wataalamu wa ngozi wanaeleza kuwa parachichi lina viini vinavoitwa ‘glutathione’ ambazo zina nguvu ya kukabiliana na ukavu katika ngozi yako.
Kwa mujibu wa mtandao unaofahamika kama www.dry-skin-guide.com, tunda hili lina uwezo wa kung’arisha sio pamoja na nywele zako.
Mtandao huo unaendelea kueleza kuwa tunda hili pia lina mafuta pamoja na vitamin B na E ambavyo ni virutubisho muhimu katika kuboresha ngozi iliyochoka na kavu.


Pia unabainisha kuwa tunda hili lina uwezo wa kupambana na bacteria na mikunjo katika ngozi yako na kurekebisha matatizo yanayochangia ukavu katika ngozi yako.
Mpaka hapo naweza kukwambia kwamba, katika suala la urembo si lazima kutumia vipodozi vya gharama ili kukidhi mahitaji ya ngozi yako. Kwa kifupi unaweza kujenga ngozi bora na yenye afya kwa kutumia matunda ambayo yanapatikana kirahisi katika mazingira yako.
Kama huwezi kuisusa ngozi yako kwa kuhofia gharama za kununua vipodozi na kama umejaribu vipodozi vya dukani bila ya mafanikio jaribu kutumia parachichi na utaona tofauti.


 Parachichi moja liloiva

 Osha ngozi yako kwa kutumia  na ikaushe kwa kitambaa safi kisha menya parachichi lako na lisage kisha lipake katika ngozi yako. Baada ya hapo acha lifanye kazi kwa muda wa dakika 15, kisha osha ngozi yako utaiona mabadliko ya ngozi yako kuwa laini na nyororo.
Waweza kutumia pia katika michirizi inayotokana na unene. Wataalamu wanaelezea kuwa matumizi ya tunda hili hayana.

Vipodozi vyenye kemikali mara nyingi husababisha kupotea kwa rangi yako asilia na vilevile husababisha ugojwa wa saratani ya ngozi ambayo mwisho wake husababisha kifo.

Wednesday, January 25, 2017

Breaking news

Nyumba imeporomoka hurumzi. Imefukia mafundi watatu mmoja kapatikana kakimbizwa hospital bado wawili wanafukuliwa

Monday, January 23, 2017

Taarifa kwa umma

TAARIFA KWA UMMA



MABALIKO YA NJIA YA DALADALA KITUO CHA GEREZANI KWA SIKU YA TAREHE 25 JANUARI 2017



Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) inawafahamisha abiria, wamiliki, madereva wa daladala na umma kwa ujumla kuwa:

·        Siku ya Jumatano tarehe 25 Januari 2017 kuanzia asubuhi hadi saa tisa alasiri kutakuwa na mabadiliko ya njia ya daladala katika kituo cha Gerezani kilichopo eneo la Kariakoo.

·        Hii ni kwa ajili ya kupisha shughuli ya uzinduzi waMiundombinu na Huduma za Mabasi yaendayo haraka  utakaofanyika siku hiyo kwenye kituo hicho.

·        Aidha kwa siku hiyo, daladala zote ambazo huishia kituo cha Gerezani zitapaswa kuishia vituo mmbadala vyaMachinga Complex na Gerezani ‘Railway Club’ kwa utaratibu ufuatao:

·        Daladala zinazotumia  Barabara ya Nyerere  na  Chang’ombe  siku hiyo zitapita Barabara ya Kawawa - Lindi hadi Machinga Complex  nakurudi kwa kutumia  Barabara ya Kawawa

·        Daladala zinazotumia  barabara ya Kilwa siku hiyo  zitaishia eneo ilipokuwa  ‘Railway Club’ na kurudi zilipotokea.

·        MUHIMU: Magari yanayoelekea Kituo cha Mnazi Mmoja yataendelea kwenda Mnazi Mmoja bila kuathirika na utaratibu huu.

·        SUMATRA inaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza



SUMATRA kwa usafiri bora na salama!

Imetolewa na:

Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini  (SUMATRA)

(Tafadhali wasambazie wengine wapate taarifa)

Safari ya dodoma yaanzia hapa.

Hiyo ni Wizara ya Utumishi leo wameeanza safari kuelekea Dodoma! Na tender wamepewa magari ya jeshi!! Kama una Lorry unasubiri


Washington kupinga urais wa Donald Trump




Maelfu waandamana Washington kupinga urais wa Donald Trump

Maelfu ya wananchi wa Marekani wanaendelea kumiminika mjini Washington kupaza sauti zao wakieleza hasira na wasiwasi wao kuhusu urais wa Donald Trump, siku moja tu baada ya kuapishwa rasmi kuwa rais wa 45 wa Marekani.


Maandamano ya Wanawake mjini Washington ambayo watayarishaji wake wanasema yatawakutanisha pamoja malaki ya watu, yana lengo ya kuwazindua Wamarekani kuhusu haki za wanawake na haki nyingine za kiraia ambazo Wamarekani wengi wana wasiwasi kwamba zinatishiwa na rais mpya wa nchi hiyo.


Trump amewakasirisha watu wengi ndani na nje ya Marekani kwa kukariri matamshi yanayowashushia hadhi wanawake, Waislamu na wahamiaji wakati wa kampeni zake za urais.




Wamarekani waandamana dhidi ya Rais Donald Trump


Maandamano ya Jumamosi ya Wanawake ambayo yalianza kwa wito uliotolewa na bibi wa Hawai katika mtandao wa kijamii wa Facebook baada ya ushindi wa Donald Trump mwezi Novemba mwaka uliopita, yanahesabiwa kuwa maandamano makubwa zaidi ya kisiasa kuwahi kushuhudiwa katika mji mkuu wa Marekani.


Wapinzani wa Rais Donald Trump wa Marekani walikuwa wakiendelea kumiminika mjini Washington kwa mabasi wakitokea katika miji na maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Richmond, Crystal Hoyt, anasema leo Wamarekani watashuhudia moja kati ya maandamano makubwa na muhimu zaidi ya kupigania uadilifu wa kijamii katika historia ya miaka 240 ya Marekani.



Profesa Crystal Hoyt ameongea kuwa, Trump ametumia siasa za kuchochea hofu, ubaguzi wa kijinsia na chuki dhidi ya wageni na wahamiaji kwa ajili ya maslahi ya kisiasa.




Maandamano ya Washington


Maandamano ya leo mjini Washington yanafanyika siku moja baada ya sherehe za jana za kuapishwa Rais mpya wa Marekani zilizoandamana na maandamano na ghasia ambazo ni kielelezo cha mgawanyiko mkubwa unaotawala jamii ya Marekani kutokana na siasa za kibaguzi za rais mpya wa nchi hiyo.


Polisi ya Washington imetangaza kuwa imewatia nguvuni waandamanaji wasiopungua 217 katika maandamano na machafuko ya jana.

Jionee majabu ya duniaa